Jina la Kitabu: لمعة الاعتقاد (Lumatul I‘tiqad )
Mwandishi: Al-Imām Muwaffaquddīn Ibn Qudāmah al-Maqdisī رحمه الله (w. 620 H)
Kitabu hiki ni miongoni mwa vitabu mashuhuri vya ‘Aqīdah ya Ahlus-Sunnah wal-Jamā‘ah. Kimeandikwa na Imamu Ibn Qudāmah, mmoja wa wanazuoni wakubwa wa madhehebu ya Hanbali. Maudhui yake yameelezwa kwa Ufupi, yakiweka wazi misingi ya itikadi sahihi ya Kiislamu.
Kinaeleza masuala ya msingi kama:
Tawhīd na sifa za Allah.
Imani kwa Malaika, Mitume, Vitabu, Qiyāmah na Qadar.
Msukumo wa kufuata Qur’an na Sunna.
Kusimama imara juu ya misingi ya Ahlus-Sunnah na kujiepusha na bid‘a.
Sheikh Shahid Muhammad alifundisha kitabu hiki mwaka 2020 katika Masjid Abeid – Mwanza, akakifafanua kwa lugha ya Kiswahili na kwa kutumia mifano halisi ya maisha ya kila siku, jambo lililowafanya wengi kufahamu aqida ya Ahlus-Sunnah kwa urahisi zaidi.