Jina la Kitabu: كشف الشبهات (Kufunua Shubha)
Mwandishi: Sheikh Muḥammad bin Abd al-Wahhāb رحمه الله
📝 Maelezo
Kitabu hiki ni miongoni mwa vitabu mashuhuri vya aqida vilivyoandikwa na Shaykh Muhammad bin ʿAbd al-Wahhāb (1115 – 1206 H). Kinaeleza kwa uwazi misingi ya Tauhidi, na kinabainisha shubha (vizingiti na hoja potofu) ambazo mara nyingi hutolewa na wapinzani wa Tauhidi. Mwandishi ameeleza shubha hizo kwa mtindo rahisi kisha akazijibu moja kwa moja kwa dalili za Qur’an na Sunna.
Ni kitabu kifupi lakini chenye maudhui yenye nguvu na kina umuhimu mkubwa kwa kila Muislamu anayehitaji kuijua dini yake kwa usahihi.
Sheikh Shahid Muhammad amekifundisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili katika Semina ya Maduati, Bukoba Mjini – Kagera, mwaka 2024, na amefafanua kwa kina shubha zote kwa uwazi na mifano ya maisha ya kila siku.